Bei za umeme kusalia vivyo hivyo mwezi huu wa Agosti
Bei za umeme zinatarajiwa kusalia bila kubadilika kwa mara ya kumi na moja mwezi Agosti huku Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Petroli (EPRA) ikiacha ushuru bila kubadilishwa.
Mdhibiti wa sekta ya nishati kwa mara nyingine tena ameacha malipo ya gharama ya mafuta (F.C.C), marekebisho ya mabadiliko ya ubadilishaji wa fedha za kigeni na ushuru wa usimamizi wa rasilimali za maji kwa sh.4.63 73 na senti mbili kwa kila uniti ya umeme inayotumiwa mtawalia.
Kusitishwa kwa ushuru huo kunatarajiwa kutilia mkazo punguzo la serikali la asilimia 15 kwa ushuru wa watumiaji, lililotekelezwa Januari mwaka huu.
Kupunguzwa kwa ushuru kulishusha gharama ya umeme kwa Wakenya kwa wastani wa asilimia 16, na hivyo kuweka gharama ya uniti 50 za umeme (saa za kilowati) kuwa sh.796.83 kufikia mwisho wa Januari.
Wakati uo huo, uniti 200 za umeme zinazotumiwa zinaendelea kutumia sh.4373.12 katika gharama katika kipindi cha ukaguzi.
Kusimamishwa kwa bei ya umeme kwa muda wa miezi minane kumesaidia kuwaepusha Wakenya kutokana na ongezeko zaidi la gharama za nishati huku bei ya bidhaa za mafuta ikipanda kwa muda uo huo.
Leave a Comment