Malkia Elizabeth wa II wa Uingereza ameaga dunia.
Kulingana na taarifa ya iliyotolewa na kasri la Buckingham, Malkia Elizabeth ameaga dunia hii leo majira ya alasiri kwenye kasri la Balmoral huko Scotland.
Haya yanakuja wakati ambapo leo malkia huyo alikuwa amewekwa chini ya uangalizi wa madaktari baada ya matabibu wake kusema wana wasiwasi na hali ya afya ya kiongozi huyo wa ufalme wa Uingereza mwenye umri wa miaka 96.
Mwanamfalme Charles ndiye mrithi wa kiti cha ufalme.
Leave a Comment