Roberto ambaye ni raia wa Mexico anasema kuwa licha ya kuwa na sifa kwa ‘kumiliki’ mshedede mkubwa, anasema hali yake imekuwa kama laana badala ya kuwa baraka kwake. Roberto mwenye umri wa miaka 58 ana mshedede wenye urefu wa inchi 18.9 kwa kiasi kwamba wanawake wanaogopa kufanya naye mapenzi.
Japokuwa amekuwa na wakati mgumu kupata mwanamke wa kufanya naye mapenzi kwa kuwa wanawake wanauogopa, amedinda kufanyiwa upasuaji kuupunguza kwa sababu unampa sifa na ufahari.
Licha ya umri wake uliosonga na ukubwa wa kifaa chake, Roberto amebaki kuwa mpweke bila mpenzi wa kurusha naye roho. Kwa mujibu wa raia huyo wa Mexico, hali yake imefanya hata kushinda kufanya kazi kwani ni mfano sasa wa ulemavu na hata yeye hutembea kwa matatizo.
Kufanyiwa ukaguzi madaktari wakamtaka kukubali kufanyiwa upasuaji lakini akadinda na badala yake kuitaka serikali kumtambua kama mlevamu na kumpa usaidizi. Jamaa huyu hana marafiki na kila anapokwenda watu hawamtaki, na huishi kwa kusaidiwa na wanajamii na kula chakula kilichomwagwa katika mapipa.
Mwaka 2011 alisafirishwa kwa lazima kutoka Marekani na serikali ya nchini hiyo hadi kwao Saltillo, Mexico na anaishi pekee yake katika chumba alichopewa na kaka zake.
Kwa mujibu wa Triplem.com, 6 January 2018, daktari ambaye alichunguza uume wake alisema kwenye matokeo kuwa ni makosa ilivyokuwa ikiripotiwa.
Cabrera aligonga vichwa vya habari kwa kudai kuwa na mtalimbo mkubwa zaidi duniani, wenye urefu wa inchi 19.
Alikabiliwa na shutuma za kudanganya kutoka kwa mwanaume mwenye uume mkubwa zaidi duniani, Jonah Falcon, ambaye alisema (Cabera) alikuwa akisambaza habari za urongo.
Madaktari wamekiri hili na kusema anaweza kuwa na maisha ya kawaida ya ngono ikiwa kimsingi atatahiriwa
Leave a Comment