Mamilioni ya Wakenya hutumia magari ya umma almaarufu matatu kuwafikisha katika sehemu zao za kazi.
Fauka ya hayo, magari hayo ya umma yanajulikana kwa kuweka vibandiko vyenye jumbe za kuchekesha.
Aidha, wahudumu wa matatu wanajulikana kwa matamshi yao ambayo mara nyingi huzua ucheshi katika steji za matatu au wanapokabiliana na wasafiri.
Hizi hapa baadhi ya jumbe za kuchekesha unazoweza kukumbana nazo katika matatu
- Mwanamume mzee kuoa msichana mdogo ni kama kununua kitabu ili wengine wapate kukisoma!
Aidha, kwa wale wenye tabia ya kusahau nauli, basi ujumbe huu utaweza kutoa tahadharisho tosha:
- Usilete stress. Kondaa ni wazimu. Dere ni moto.
Pia kuna ujumbe wa kumtahadharisha afisa wa polisi anayepanda matatu:
3. Si Makosa Karao (afisa wa polisi) Kulipa Gari
4. Ukiona kuna jam kubwa nunua blueband
5. Hatusemi wewe ni mnene lakini ukikalia viti viwili lipa.
6. Kama lazima ukae mbele shukisha dereva.
7. Fare haijapanda ni wewe umesota
8. Ukiskia gari liko na joto shuka upande fridge.
9. Hakuna stage ya ashu (KSh 10), nunua avocado teleza hadi town
10. Kama sketi za shule zakuchanganya kamshonee mkeo
Leave a Comment